NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

CHANGA MOTO HUDUMA YA AFYA ILEMELA, SERIKALI YAWAONYA WAHUDUMU



Serikali yawaonya wahudumu wa afya Ilemela
SERIKALI kupitia Idara ya Afya, Wilaya ya Ilemela, Mwanza imewaonya wahudumu wa afya wanaofanya kazi kwa mazoea badala ya kutumia weledi wao katika kuihudumia jamii ili kuepusha vifo visivyo vya lazima.
Onyo hilo lilitolewa juzi jijini Mwanza na Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Desderius Polle wakati akifungua semina iliyoandaliwa na Chuo cha Mafunzo na Maendeleo (MC TCDC) chini ya ufadhili wa hospitali ya Aga Khan, kupitia mradi wa Joining Hands Initiative (JHI).
Semina hiyo imewashirikisha wahudumu mbalimbali wa afya kutoka kata mbili za Pamba na Butimba jijini hapa.
Polle ambaye pia ni Ofisa Afya wa Ilemela, alieleza kuwa wahudumu wa afya ni muhimu katika ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa, hivyo ni vema wataalamu hao watimize wajibu ipasavyo.
Awali mkufunzi wa mafunzo hayo, Joram Masesa aliwasihi wauguzi wote kutekeleza vema majukumu yao ili kuokoa uhai wa mama na mtoto.
Kwa mujibu wa Masesa, vifo vya wanawake vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga chini ya miaka mitano lazima vitokomezwe ili kujenga jamii salama.

0 comments: