NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

RAISI KIKWETE AZIDI KUTIMIZA AHADI ZAKE NA ZA CHAMA CHA MAPINDUZI


Rais Kikwete aendelea kutekeleza ahadi zake na ilani za chama cha mapinduzi, azindua daraja la Mwanhuzi, mikoa mitatu       kunufaika


                                                                     
AHADI ya ujenzi wa daraja la Mwanhuzi wilayani Meatu, Simiyu imetimia baada ya Rais Jakaya Kikwete kulifungua rasmi, baada ya ujenzi wake kukamilika na kuanza kutumika.
Kabla ya kulifungua daraja hilo, Rais Kikwete aliwaasa wakazi wa Mwanhunzi na watumiaji wengine kulitunza daraja hilo na kuhakikisha huduma ya usafiri kati ya Meatu na mikoa ya Arusha na Singida inakuwepo.
“Ninawasihi mlitunze daraja hili na asije akatokea mtu kwenda kuanza kukata vyuma au kunyofoa vifaa vingine vya daraja, kwani kufanya hivyo mtadhohofisha ubora wake.
“Likiharibika kabisa tukajikuta tunarudi kwenye kero ya usafiri wa eneo hili kama ilivyokuwa kabla ya kujengwa daraja hili,” alisisitiza rais.
Daraja hilo lenye urefu wa mita 40 ni kiungo muhimu cha kuvuka Mto Mwanhuzi ilipo barabara kuu itokayo Kolandoto mkoani Shinyanga kupitia Lalago mkoani Simiyu na kuelekea Singida na Arusha.

0 comments: