NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

MSHINDI WA EBSS, MWANZA KWA MARA NYINGINE YAZIDI KUNG'ARA YAZUA GUMZO KUBWA

Emmanuel Msuya kutoka ILEMELA Mwanza ndie mshindi wa Epiq Bongo Star Search 2013
 Mkurugenzi wa Bench Mark Production na Chief Judge wa shindano la Epiq Bongo Star Search Madam Ritha Paulsen (kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Kampuni ya simu za mkononi Zantel Bw. Ali Bakari kwa pamoja wakimkabidhi sanduku lenye  kitita cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania Mshindi wa shindano hilo Emmanuel Msuya ambae ni kijana kutoka Ilemela MWANZA. Mkoa wa MWANZA alimaarufu kama 'ROCKY CITY' unazidi kuibua vipaji mbalimbali nchini Tanzania, na hii ni mara ya pili kutoa mshindi wa BSS tangu mshindi wa BSS mwaka 2009 Pascal Casian. Shindano hilo ambalo ni chuo cha muziki kwa hapa nchini ambalo kwa sasa ni maalufu kwa jina la EBSS imetoa wanamuziki maalufu nchini na Afrika kama vile Peter Msechu, Pascal Casian ambae kwa sasa anafanya ziara mbalimbali za kimuziki barani Ulaya na Asia, Baby Madaha, Walter, Kala Jeremiah anae tamba na wimbo wake wa HIP POP uitwao Dear GOD, Jumanne Idi, Abubakhari Mzuri na wengine wengi. Mshindi wa EBSS 2013 Emmanuel Msuya amejinyakulia Tshs. 50,000,000/- taslimu.

Meza kuu ya Majaji wa shindano la Epiq Bongo Star Search, walikuwa ni Chief Judge Madam Ritha Paulsen, Msanii wa muziki nchini Banana Zoro pamoja na Joachim Kimaro a.k.a Master J wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye fainali za shindano hilo lililofanyika mwishoni mwa Juma kwenye fukwe za kiota cha Escape One, Mikocheni jijini Dar. Mshindi wa EBSS 2013 ni Emmanuel Msuya kutoka Mwanza na nafasi ya pili ilichukuliwa na Elizabeth Mwakijambile.



0 comments: