NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

HONGERA DR. ASHA-ROSE MIGIRO. M/KITI WETU TAIFA AMEKUAMINI NA SISI PIA TUNAKUAMINI

                                            (NAPE NNAUYE AKIMPONGEZA DR. ASHA-ROSE MIGIRO BAADA YA KUTEULIWA KUWA MBUNGE.)
Naibu katibu mkuu mstaafu wa umoja wa mataifa  na pia ni katibu wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (NEC) siasa na kimataifa Dr. Asha-Rose Migiro. Jana aliteuliwa rasmi na raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania amabae pia ni mwenyekiti wa chama cha  mapinduzi taifa Dr. Jakaya Kikwete kuwa mbunge wa bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania anaeteuliwa na raisi. Kwamujibu wa katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania, raisi anamamlaka ya kuteua wabunge kumi na kuwafanya kuwa miungoni mwa wabunge wa bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania. Kwa kufanya hivyo  Mh. Kikwete ameonyesha jinsi gani alivyomuamini na kuukubali utendaji na uwajibikaji wa Dr. Asha-Rose Migiro tangu alipo kuwa akifanya kazi za umoja wa mataifa(UN). Lakini pia Mh. Raisi ameonyesha jinsi gani anavyo waamini akina mama wote wa Tanzania pamoja na mchango wao katika jamii na maendeleo ya nchi yetu.
Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi wilaya ya Ilemela na mkoa wa Mwanza kwa ujumla unampongeza Dr. Migiro kwa kuaminiwa na Mh. Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuwa miungoni mwa wabunge  wa bunge letu la Tanzania. Chama cha mapinduzi ni chama cha watu wa aina zote, wanaume kwa wanawake, vijana kwa wazee na pia ni chama cha makabila na dini aina zote. Kidumu chama cha mapinduziiiiii, Kidumu chama tawalaaa!!!!

0 comments: