NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

SERIKALI YABARIKI UCHAGUZI WA MEYA NA NAIBU MEYA ILEMELA. WAZIRI GHASIA AFAFANUA. WASHINDANI WANYAMAZISHWA.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi). Hawa Ghasia amethibitisha kuwa uchaguzi huo wa Meya na Naibu meya wa wilaya ya Ilemela ulikuwa wa haki na akidi ilikamilika. Ghasia alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Nyamagana Hezekiah Wenje juzi bungeni aliyetaka serikali kutoa tamko la kufuta uchaguzi huo. Hata hivyo  Waziri Ghasia aliendelea na msimamo wake kwamba akidi katika uchaguzi huo ilitimia hivyo viongozi waliochaguliwa ni halali. Licha ya kuwa  uchaguzi huo ulihudhuriwa na madiwani 6 kati ya 14, lakini bado ni halali kutokana na wajumbe 3 wa baraza la madiwani kufungiwa kwa muda wa miezi 3 kwa kosa la kudharau amri halali ya mahakama  na wengine 5 kugoma kuhudhuria mkutano huo pamoja na kupatiwa taarifa na Mkurugenzi. ‘‘Wajumbe 6 walifanya uchaguzi huo ni halali kwa kuwa ulihudhuriwa na zaidi ya nusu ya wajumbe halali walio paswa kuhudhuria kikao hicho ambao walitakiwa kuwa 11’’ aliseama Waziri Hawa Ghasia. Kwamujibu wa maelezo ya Waziri Hawa Ghasia Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Mh. Henry Matata na Naibu Meya Mh. Swila Dede Swila wapo kihalali na hakuna utata tena juu ya hilo.

0 comments: