NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

KIGOMA YAONYESHA HATIMA YA CHADEMA. KATIBU MKUU SLAA APOKELEWA NA WATU WACHACHE HASA WATOTO.


Kwakweli kila lenye mwazo halikosi kuwa na mwisho. Kipimo kikuu cha maendeleo huwa ni kutoka 0-1000 nasio 100-10. Hii ni hesabu rahisi sana kwa watu wenye busara na hekima lakini kwa watu walio na upeo mdogo wakuelewa kamwe hawatanielewa nini kinamaanishwa hapa. Mwanzoni walipo kuwa wakiitisha mikutano watu wengi walijitokeza kutaka kuwasikiliza mamia kwa maelfu wazee kwa vijana, waume kwa wanawake, watoto kwa wakubwa wote walikua wakikusanyika kwa pamoja  katika viwanja husika. Leo mambo yameanza kubadilika, mahudhurio kwa wafuasi yameshuka kwa kasi ndani ya mda mfupi sana hasa baada ya kumvua uongozi alie kuwa naibu katibu mkuu wa CHADEMA taifa Zitto Kabwe. Hii inaonyesha ni jinsi gani chama kilivyo mikononi mwa watu nasio mioyoni mwa watu. Kiukweli hali ya hewa sio nzuri kwa ndugu zetu ila wanajikaza tu ili kuficha aibu yao. Hata siku moja huwezi kumfukuza mtu katika nafasi furani tena kwa vitisho alafu baadae urudi kwenye jimbo lake au kwa wapiga kula wake ili kuzidi kumchafua halafu wakusikilize wakati wao hawaoni kosa. Wakikuheshimu sana wataondoka wala hawata kuja kukusikiliza kamwe na ukizidi kuwasumbua watakupiga. Hivi ndivyo ilivyokuwa mkoa wa Kigoma siku chache zilizopita wakati katibu mkuu wa CHADEMA Dr.Slaa alipoenda kuzulu katika mkoa huo na kupokelewa na watu wachache hasa wengi wao wakiwa watoto kama picha inavyo honyesha na si vinginevyo. Katibu mkuu huyo alizidi kuwakera watu zaidi pale aliposema wanaomlilia Zitto waondoke naye. Haya hayakuwa maneno mazuri sana ya kuongea mbele ya wapiga kula na wana chama wa mbunge husika. Kweli hali hii sio nzuri.   

0 comments: