NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

HOTUBA YA RAISI KIKWETE NCHINI A.KUSINI KATIKA MAZISHI YA MADIBA IMETUNG'ARISHA WATANZANIA. WASOUTH WATOKWA MACHOZI YA FURAHA.


Hotuba ya Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete imezidi kujenga na kuimarisha uhusiano wa Tanzania na Afrika kusini. Kupitia hotuba yake nzuri Raisi Kikwete ameeleza kwa undani zaidi jinsi nchi ya Tanzania ilivyo husika kwa sehemu kubwa kuhakikisha Afrikakusini inapata demokrasia ya kweli na kuondoa ubaguzi wa rangi uliokuwa umeshamiri katika nchi hiyo. Lakini pia Raisi Kikwete  alielezea jinsi gani Mwl. Nyerere alivyo mpokea Mzee Mandela alipoondoka kwa siri kutoka Afrika kusini kuja Tanzania bila kuwa na hati za kusafiria, lakini alipewa hati hizo na Tanzania na kusafiri katika nchi za Ghana, Algeria na Ethiopia kama mtanzania. Raisi Kikwete aliongelea pia uhusiano mzuri na wakaribu kati ya chama tawala cha Afrika kusini ANC na chama tawala cha Tanzania CCM ulivyo imara.  Raisi Kikwete alieleza jinsi gani watanzania wameguswa na msiba huu wa Madiba na kusistiza kuwa tupo  pamoja katika kipindi hichi kigumu cha msiba wa Dunia nzima kwa ujumla.
TUNAKUPONGEZA RAISI KIKWETE KWA KUIKUMBUSHA DUNIA JINSI GANI WATANZANIA TULIVYO WAKARIM NA JINSI GANI TULIVYO NA UPENDO KWA MAJIRANI ZETU.

0 comments: