NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

MBOWE ATUMIA GARI LA KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI (SERIKALI) KATIKA MIKUTANO YA CHADEMA. Hizi ni picha halisi


Hili ni gari linalo tumiwa na kiongozi mkuu wa upinzani Bungeni. Ni gari linalo milikiwa na serikali ya Tanzania inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi kwa kutumia kodi halali za wananchi wa vyama vyote. Chaajabu gari hili limeonekana katika shughuli za kisiasa za CHADEMA katika mkutano uliofanyika maeneo ya Nyegezi Malimbe katika viwanja vya shule ya msingi nyamalango na kuhudhuriwa na mwenyekiti wa chama hicho taifa Bw. Freeman Mbowe kama msemaji mkuu wa mkutano huo. Nikitu kisicho ruhusiwa kwa kiongozi yeyote wa serikali au chama chochote cha kisiasa kutumia gari la serikali katika shughuri zozote  zile zinazohusu chama cha kisiasa. Ukweli ni kwamba kama jambo hili lingefanywa na kiongozi wa chama kingine cha kisiasa kama CCM wanachama wa upinzani hasa CHADEMA na viongozi wao wangelalamika na kuliita jambo hilo kuwa ni matumizi mabaya ya mali za uma, lakini wao wameliona jambo hilo kama ni halali. Jambo hili linaonekana kama ni moja ya ufisadi wa kichini chini unaofanywa na kiongozi mkuu wa upinzani Bungeni kwa kushindwa kutumia gari za chama chake katika shughuri zinazo husu siasa na chama chake badala yake anaanza kutumia gari la serikali linalopaswa kutumika katika shughuri za serikali tu.

0 comments: