NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

WASIRA NA NGEREJA WAWAFURAISHA WANAFUNZI WA SAUT. NIKATIKA KONGAMANO LA MIAKA 52 YA UHURU LILILOANDALIWA NA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU MKOA WA MWANZA.


Wageni waalikwa waliwasili mapema saa 6 na nusu mchana. Wageni rasmi walikua ni M/kiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza Ndg. Antony Diaro, MNEC anaewakilisha wilaya ya Sengerema  na Mbunge wa wilaya hiyo pia Ndg. William Ngereja. Mgeni mwingine alikuwa ni Mb. Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Ndg. Steven Wasira.  Wakiambatana na wageni wengine kama M/kiti wa UVCCM Ilemela Ndg.Kheri James, M/kiti wa UVCCM Nyamagana na Wengine wengi.
Katibu mwenenezi wa tawi la Kambarage SAUT aliwakaribisha wageni wote na kumkaribisha katibu wa CCM wilaya ya Nyamagana ambaye naye alimkaribisha M/kiti wa tawi la kambarage kwaajiri ya kumkaribisha Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza kwaajiri ya kumkaribisha M/kiti wa CCM mkoa wa Mwanza Ndg. Antony Diaro kufungua kongamano rasmi naye alifanya hivyo na kongamano lilianza kama ilivyokua imepangwa. Mgeni rasmi alitoa hotuba nzuri naya kuvutia huku akikazia sana suara la watu kutokukubari kudanganywa na watu wachache wanao potosha ukweli wa mambo. Baada ya hotuba mambo mengine yaliendelea.
M/kiti wa tawi la Kambarage alimkaribisha mtoa mada no.1 Ndg. Mwl. Julius Lugendo kwa ajiri ya kutoa na kuielezea mada iliokua inahusu Harakati za ukombozi wa taifa letu kuanzia mwaka 1905 mpaka ukombozi ulipo patikana mwaka 1961. Mtoa mada huyo alihitimisha kwa kusema ni lazima kila mtu ailinde na kuitunza amani tulionayo kwasababu ilipatikana kwa gharama kubwa sana ilio husisha maisha ya watu wengi.
M/kiti wa tawi la Kambarage alimkaribisha mtoa mada no.2 Ndg. Steven Wasira ambaye ni Waziri Ofisi ya Raisi uratibu mahusiano na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM kwaajiri ya kutoa na kuielezea mada aliyopangiwa. Mada hiyo ilikua inahusu Mstakabali wa serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na uwepo wa serikali tatu. Mh. Wasira alielezea vizuri kuhusu mada hiyo hasa akikazia gharama ambazo Tanganyika itazipita baada ya muundo huo wa serikali tatu. ‘‘ Tanganyika au Tanzania bara ndio itakayo beba gharama zote za serikali tatu hizi kwa vile ndio inauchumi mkubwa na ina vyanzo vingi vya mapato ukilinganisha na Zanzibar hivyo sio jambo zuri sana la kuling’ang’ania kwa sababu lazima muungano wetu uliodumu kwa miaka 50 utavunjika kwa vile Tanganyika aitaweza kukubali kubeba gharama zote hizo’’ alisema Waziri Wasira pamoja na mambo mengie mengi. Mwisho Waziri Wasira alisisitiza swala la uzalendo na kujijua miongoni mwa vijana wachapakazi wa Tanzania.
Baada ya mtoa mada no.2 kumaliza M/kiti wa tawi la Kambarage alimkaribisha mtoa mada no.3 Ndg. Peter Begga amabaye alikuja kuelezea mada iliyokua inaeleza mafanikio ya taifa letu katika Nyanja ya elimu. Ndg. Peter Begga alielezea vizuri kiwango cha elimu kilichokuwepo wakati Tanganyika inapata uhuru na sasa. Wakati Tanzania inapata uhuru ilikuwa na wanafunzi 14 tu wa chuo kikuu lakini sasa ni zaidi ya laki moja na nusu. Peter Begga alimaliza kuongelea mada yake vizuri na kuzidi kuwasisitiza wanafunzi wa chuo kikuu kufuata maadili ya kielimu na kuwa tofauti na watu ambao hawajasoma ili kuwa mifano mizuri ya kuigwa.
M/kiti wa tawi la Kambarage alimkaribisha Mbunge na MNEC anayewakilisha wilaya ya Sengerema Ndg. William Ngereja ambaye alisimama kuielezea mada yake iliyokua inahusu Nafasi ya Vijana katika ujenzi wa taifa. Mh. Ngereja alieleza kwa makini jinsi vijana wanavyo pewa nafasi ya mbele na serikali yao kwa vile vijana ni zaidi ya 65% ya wananchi wote watanzania. Mh. Ngeraja aliwataka vijana wote hasa wasomi wa vyuo vikuu kutokukubali kutumiwa na Wanasiasa wasiokuwa na huruma na taifa lao. Waziri huyo wa zamani wa Nishati na Madini alizidi kuwaomba vijana wazidi kufanya kazi kwa nguvu zaidi ili wajikwamue kiuchumi na wanaosoma wazidi kusoma sana ili kujenga taifa la wasomi hodari. Hivi ndivyo Mh. Ngereja alivyomaliza kutoa na kuielezea mada yake.
Hivi ndivyo mambo yalivyokuwa jana katika mahadhimisho ya miaka 52 ya uhuru wa Tanzania yaliofanyika jana katika ukumbi wa mwanza sekondari hapa jijini Mwanza

0 comments: