NEWZZZZ...........

THE VOICE OF UVCCM ILEMELA MWANZA
MWENYEKITI WA UVCCM ILEMELA COMRED KHERI .D. JAMES

WAAFRIKA KUSINI WAIBARIKI TANZANIA. NI BAADA YA KUGUNDUA UKOMBOZI WAO ULIANZIA TANZANIA. WENGI WALIKUA HAWAJUI. WAMKUMBUKA TENA NYERERE.


UHUSIANO baina ya Tanzania na Nelson Madela ulichochewa na mauaji ya Sharpeville yaliyotokea mwaka 1960; na ulipita katika majaribu mengi yakiwamo mkutano baina ya Madiba na Mwalimu Nyerere mwaka 1962.
Mapitio ya maandishi mbalimbali pamoja na mahojiano ambayo gazeti hili limefanya na watu waliofahamu uhusiano baina ya Mandela, Nyerere, nchi pamoja na vyama vyao, yameeleza mengi kuhusu uhusiano huo wa kihistoria baina ya nchi hizi.
Maandishi katika mtandao wa chama tawala cha ANC cha Afrika Kusini, yanaonyesha namna uongozi wa juu wa chama hicho ulipoamua kuhamia Tanganyika baada ya serikali dhalimu ya makaburu wa Afrika Kusini kukipiga marufuku chama hicho pamoja na kile cha PAC, baada ya mauaji hayo ya Sharpeville.
Chama hicho kilimtuma kada wake, Frene Ginwala, kuja nchini hapa mwaka huo huo wa 1960 na yeye ndiyo hatimaye aliyepanga mipango ya kuwasafirisha kwa siri viongozi wa juu wa ANC kama vile Oliver Tambo na Yusuf Dadoo kuja Tanganyika wakati huo.
Baadaye, Ginwala alipewa kazi na Mwalimu Nyerere kama mhariri wa gazeti la serikali la Standard (sasa Daily News) na Baba wa Taifa ndiye aliyewapokea akina Tambo na huo ndiyo ukawa mwanzo wa uhusiano wa kipekee baina ya Tanzania na wapigania uhuru wa Afrika Kusini.
Chama cha ANC kinasema kwamba wakati chama hicho kilipoamua kutumia nguvu kuung’oa utawala wa makaburu, kilimtuma Mandela kuja Tanganyika ili kuzungumza na Nyerere kwa ajili ya kupewa msaada wa kifedha na mafunzo.
“Hata hivyo, mkutano huo wa kwanza baina ya Nyerere na Mandela haukuisha vizuri kwa sababu Mwalimu aliwataka ANC kusitisha njia ya mapigano hadi kwanza utawala wa makaburu utakapomtoa gerezani mpigania uhuru mwingine wa chama cha PAC, Robert Sobukwe.
“Nyerere pia alikuwa na uhusiano mzuri na Sobukwe na kwa kweli Mandela hakufurahishwa sana na ushauri huo wa Nyerere. Hata hivyo, katika miaka iliyofuata uhusiano huo, Tanzania ilikuja kuwa mshirika mzuri sana wa ANC,” unasema mtandao wa www.sahistory.org.za
Taarifa rasmi zinaeleza kwamba Tanzania ndiyo yalikuwa makao makuu ya kwanza ya ANC na PAC na hadi kufikia mwaka 1965, jumla ya wapigania uhuru 800 walikuwa wanapata mafunzo katika vyuo vya Mazimbu, mkoani Morogoro na Kongwa mkoani Dodoma.
Mazimbu na Kongwa
Nyerere, baadeye kubali kuanzishwa kwa kambi ya kwanza ya mafunzo ya kijeshi ya wapiganaji wa kundi la Umkhonto wa Sizwe wilayani Kongwa mkoani Dodoma kati ya mwaka 1963 na 1964 na serikali ya Tanzania ilikuwa ikigharamia sare na mlo mmoja wa wapiganaji hao.
Miongoni mwa walioanzisha kambi hiyo ni Joe Modise ambaye baadaye alifikia kuwa Waziri wa Ulinzi katika serikali isiyokuwa ya kibaguzi ya Afrika Kusini.
Kambi ya Mazimbu ndiyo ambayo baadaye ilikuja kujenga chuo cha mafunzo maarufu kwa jina la Solomon Mahlangu (SOMAFCO).
Maelezo mbalimbali yanaonyesha kwamba aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Moroagoro katika miaka ya 1970, Anna Abdallah (baadaye alikuja kuwa waziri katika wizara mbalimbali na sasa mbunge), ndiye aliyewapa eneo hilo wapiganaji hao wa ANC.
Nusura uhusiano uvunjike
Mwaka 1969, uhusiano baina ya ANC na Tanzania ulifikia katika hatua mbaya. Kada wa TANU, Oscar Salathiel Kambona, alidaiwa kutaka kumpindua Nyerere kwa kushirikiana na wapiganaji wa Umkhonto waliokuwa wamechoka kufanya mazoezi hapa nchini pasipo kutumwa kurudi kwao kuanzisha mapambano.
Maelezo kuhusu hilo yalitolewa na kada wa PAC, Potlako K. Lebalo, na serikali ya TANU iliamua kurejesha makambini wapiganaji wote wa ANC waliokuwepo ikiwa ni pamoja na kukiondoa chama hicho hapa nchini.
Hata hivyo, mwana historia wa ANC, William Gumede, anasimulia kwamba Tambo aligoma kulazimishwa kwa wapiganaji hao kufungiwa makambini; kwa maelezo kwamba wao ni “Wapigania Uhuru na si wakimbizi.”
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa ANC kuhamishia Lusaka makao yake makuu ambayo yalidumu hadi chama hicho kiliporuhusiwa tena kushiriki katika siasa.
Hata hivyo, serikali ya Tanzania ilikuwa na msimamo mkali pia dhidi ya wanachama wa ANC waliokuwa na mrengo wa kikomunisti. Hiyo ndiyo sababu wanachama kama Michael Harmel, Dadoo, Joe Slovo na Ruth First baadaye walipigwa marufuku kukanyaga katika ardhi ya nchi hii.
Hata hivyo, kutokana na mauaji ya Soweto ya mwaka 1976, ambayo pia yalisababisha utawala wa makaburu kukamata watu wengi zaidi, ndipo wananchi wengine wakakimbia Afrika Kusini na kuja Tanzania.
Hapo tena, Anna Abdallah, kwa maelekezo ya Nyerere, alitafuta eneo katika mkoa wake kule Dakawa ambako nako ikawa kambi ya wapiganaji.
Alipotoka jela, Mandela kwanza alitembelea Lusaka yalikokuwa makao makuu ya ANC na ndipo akafanya ziara yake ya kwanza nchini Tanzania ambapo alipokewa na Mwalimu aliyekuwa amestaafu tayari.
HEKIMA NA BUSARA ZA BABA YETU NYERERE ZITATUTANGAZA VEMA MPAKA MWISHO WA DUNIA.

0 comments: